Maisha Marefu huja kwa Kuutunza Mwili

Maisha Marefu huja kwa Kuutunza Mwili
Fanya Mazoezi kulinda Afya yako

Ijumaa, 10 Aprili 2015

Maana ya kalori(Calories) katika mwili



Kalori ni kipimo cha nishati, katika lishe na lugha ya kawaida, Kalori ni matumizi ya nishati katika chakula na vinywaji na matumizi ya nishati ya mwili katika shughuli za kawaida za mwili. Kwa mfano, tunda la apple linaweza kuwa na kalori 80, lakini kutembea kilomita moja kunaweza kutumia mpaka kalori 100
Aina za kalori:


·         Kalori ndogo (Alama :cal)- ca 1 ni kiasi cha nishati kinachohitajika kunyanyua gramu moja ya maji kwa digrii moja ya Celsius.

·         Kalori(Alama: kcal)- Kca 1 ni kiasi cha nishati kinachohitajika kunyanyua kilogramu moja ya maji kwa digrii moja ya Celsius

Watu wengi wanakosea wanapohusianisha Karoli katika chakula na vinywaji, lakini kitu chochote kilicho na nichati kina kalori. Kwa mfano tani moja ya makaa yam awe inaweza kuwa sawa na kalori 7,004,684,512

Kalori kubwa 1= kalori ndogo 1000

Kalori ambazo huandikwa katika lebo za vyakula, huwa, kilokalori ambazao huwa na kiasi cha kalori ndogo 1000


Kwa nini kalori ni muhimu  kwa afya ya binadamu?
Mwili wa binadamu unahitaji nishati ili uweze kuwepo katika hali ya kawaida, bila nishati katika mwili chembe hai katika mwili huweza haribika na kufa, ikiwa hivyo moyo na mapafu vinaweza simama kufanya kazi zake.  Mwili unapata nishati kutoka katika vyakula na vinywaji.
Kama tutatumia kiasi cha kalori ambacho mwili unahitaji kila siku, hakika utafurahi kuwa na afya njema. Lakini matumizi ya kalori katika mwili yapo chini sana au juu sana, bila shaka utapata matatizo ya kiafya.
Kiasi cha Kalori ambacho kimo katika chakula ni kiasi kinachotuonyesha nishati iliyomo katika chakula hicho. Hapa chini kuna vipimo vya kalori katika aina kuu za
vyakula tunavyokula.
  • Gramu 1 ya wanga(carbs) ina kiasi cha kalori 4
  • Gramu 1 ya protini ina kiasi cha kalori 4
  • Gramu 1 ya mafuta(fats) ina kiasi cha karoli 9

Kiasi gani cha kalori tunahitaji katika siku?
Si kila mtu anahitaji kiasi kile kele cha kalori  anachotumia siku moja katika siku zote. Mahitaji yetu ya kalori katika mwili yanategemea mambo mbalimbali ikiwamo afya ya mwili kiujumla, mahitaji ya mwili katika shughuli/kazi, jinsia, uzito, kimo na umbile. Mfano mchezaji wa mpira wa umri wa  miaka 25 mwenye urefu wa futi 6 anahitaji kalori nyingi zaidi kuliko mwanamke wa miaka 50 mwenye urefu wa futi 5.
Mamlaka za afya mbalimbali duniani bado hazijakubali kuhusu kiasi ambacho watu wao wanatakiwa watumie, mfano Marekani wao wanashauri kwamaba mwanaume anatakiwa atumie kwa wastani kalori 2700 kwa siku na mwanamke atumie wastani kalori 2200 kwa siku, wakati Uingeraza(nationa Health Service) wanashauri ni 2500 na 2000 kwa mwanamke.
Wakati huo huo shirika la Kilimo na Chakula Duniani(FAO) linasema mtu mzima anatakiwa asitumie chini ya kalori 1800 kwa siku.

0 comments:

Chapisha Maoni

Machapisho Maarufu

Kumbukumbu

Inaendeshwa na Blogger.