Maisha Marefu huja kwa Kuutunza Mwili

Maisha Marefu huja kwa Kuutunza Mwili
Fanya Mazoezi kulinda Afya yako

Mazoezi



Mazoezi ya mwili


Mazoezi ya mwili nishughuli yoyote ambayo inayouwezesha mwili kuwa na utimamu wa mwili siha na afya njema ya mwili kiujumla  katika utendaji wake. Hivyo ufanywaji wa mazoezi ya mwili hufanyika kwa madhumuni ya kuboresha  na kukarabati mifumo mbalimbali katika mwili ili iweze kufanya kazi inavyotakiwa, kuboresha ujuzi wa kimichezo na kuburudisha mwili na akili.
Faida za mazoezi ya Mwili
Mazoezi ya mwili ya mara kwa mara yanasaidia katika mambo yafuatayo kama
·        Kuboresha mfumo wa kinga mwilini
·        Kupunguza magonjwa ya moyo na kuboresha utendaji wa mfumo wa moyo na damu(CARDIOVASCULAR SYSTEM)
·        Kupunguza magonjwa ya mapafu na kuboresha mfumo wa mapafu(PULMONARY SYSTEM)
·        Kuzuia magonjwa ya kisukari hasa ugonjwa kisukari namba 2(type 2 diabet)
·        Kupunguza tatizo la unene kupita kiasi au kiribatumbo (obesity)
·        Kuboresha afya ya akili na utendaji kazi wa ubongo
·        Kupunguza msongo wa mawazo na mfadhaiko
·        Kumwezesha mtu kuwa na hali ya kujisikia kwa kuwa na afya nzuri(self esteem)
Kwa ujumla mazoezi yanafaida nyingi sana hasa katika kipindi hiki ambacho mfumo wa maisha ya watu umebadilika na kupunguza utendaji kazi wa mwili wa kiasili kutokana na vyakula na shughuli za kibinadamu hivyo kusababisha kiribatumbo/uzito na magonjwa mengine hatari.

Aina za mazoezi
Mazoezi ya mwili yamegawanyika katika makundi matatu kutokana na matokeo mwili yanayofanyika katika mwili pindi mazoezi hayo yanapofanyika

1.      Mazaoezi ya Aerobiki (Mazoezi yanayohusisha Oksijeni nyingi)
Mazoezi haya huusisha shughuli yoyote ambayo inatumia misuli mingi ya mwili na kusabaisha matumizi makubwa ya oksijeni mwilini tofauti na hali ya kawaida .

Malengo makubwa ya mazoezi haya ni kuongeza ustahimilivu wa utimamu wa mfumo wa Moyo/mzunguko wa damu na mfumo wa Mapafu/hewa.
Mfano wa mazoezi ya Aerobiki ni: kuendesha baiskeli, kuogelea, kutembea kwa kasi, kukimbia, kuruka na kuvuta kamba, mazoezi ya viungo ya mwendelezo pamoja na michezo mbalimbali kama mpira wa miguu, tenisi n.k
2.      Mazoezi ya Anaerobiki (Mazoezi yasiyohusisha matumizi ya Oksijeni nyingi)
Aina hii ya mazoezi huitwa mazoezi ya nguvu au ukinzani katika mwili ambapo huwezesha kuipa nguvu na  uimara  misuli na mifupa , kuratibisha uwiano wa mwili na uratibu wa mfumo wa misuli.
Mfano wa mazoezi haya ni: Mazoezi ya Msukumo(pushups), Mchuchumio(lunges), kujivuta(pull-ups), kukimbia kasi(sprintings), kunyanyua na kuvuta vitu vizito(weightlifting and rowing)
3.      Mazoezi ya Mnyumbuko(Flexibility)
Mazoezi ya Mnyumbuko ni aina ya mazoezi ambayo huusisha unyumbuaji au uvutaji wa misuli katika mwili ili kuwezesha ubadilikaji wa umbo la misuli katika mwili unapofanya kitu chochote, mazoezi haya hupunguza majeraha katika misuli pindi tendo lolote la kiutendaji la mwili katika mwendo linapofanyika.

Kwa ujumla mazoezi ya mwili yanawezesha umakini(accuracy), wepesi wa mwili(agility), nguvu(power) na Mwendokasi(speed) katika shughuli za kawaida za binadamu na michezoni.


0 comments:

Chapisha Maoni

Machapisho Maarufu

Kumbukumbu

Inaendeshwa na Blogger.